100.Surat Al-A'adiyaat |
Imeshuka Makka | Ina aya 11 |
Utangulizi | Orodha ya Sura | Faharasa |
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0
1. Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,
1
2. Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,
2
3. Wakishambulia wakati wa asubuhi,
3
4. Huku wakitimua vumbi,
4
5. Na wakijitoma kati ya kundi,
5
6. Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
6
7. Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
7
8. Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
8
9. Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
9
10. Na yakakusanywa yaliomo vifuani?
10
11. Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na
khabari zao wote!
11
Sura Nyingine | Faharasa |