105.Surat Al-Fiil |
Imeshuka Makka | Ina aya 5 |
Utangulizi | Sura Nyingine | Faharasa |
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0
1. Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye
tembo?
1
2. Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?
2
3. Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi,
3
4. Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni,
4
5. Akawafanya kama majani yaliyo liwa!
5
Sura Nyingine | Faharasa |