Kwa jina la Mwenyeezi Mungu Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu
Utangulizi:
Rudi kwenye sura
* 1. Hakika, ewe Muhammad, unajua kwa ujuzi usio ingiliwa na shaka yoyote,
alivyo fanya Mola wako Mlezi kuwafanyia wale watu wenye tembo (ndovu), wakataka kuishambulia
Nyumba takatifu ya Al-Kaaba.
Rudi kwenye sura
* 2. Unajua ya kwamba hakika Mwenyezi Mungu amejaalia juhudi yao kutaka
kuibomoa Al-Kaaba ivize na ipotelee mbali. Juhudi yao ikapeperuka, na wao wasipate makusudio yao.
Rudi kwenye sura
* 3. Na Mwenyezi Mungu aliwasalitisha na majeshi ya ndege yaliyo watokea
makundi kwa makundi yakifuatana, na yakawazunguka kila upande.
Rudi kwenye sura
* 4. Wakiwatupia mawe kutoka Jahannamu.
Rudi kwenye sura
* 5. Akawafanya kama majani ya mimea yaliyo sibiwa yakatilifu.
Rudi kwenye sura
Copyright © 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani